Mh. Lowassa aipongeza kampeni ya hoteli ya Double Tree kwa kutoa taa za nishati ya jua - Arusha Forum
Headlines News :
Home » » Mh. Lowassa aipongeza kampeni ya hoteli ya Double Tree kwa kutoa taa za nishati ya jua

Mh. Lowassa aipongeza kampeni ya hoteli ya Double Tree kwa kutoa taa za nishati ya jua

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Friday, May 31, 2013 | 1:19 PM

Mkurugenzi wa Kanda wa Hoteli ya DoubleTree by Hilton ya Dar es Salaam Bw. Judd Lehmann akifafanua jambo kwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli Mh. Edward Lowassa (kulia) ambapo amemweleza kuwa huu ni mwendelezo wa Kampeni yao itakayodumu kwa takribani miaka miwili tangu walipoanza na lengo likiwa nikuwafanya wanafunzi hususani wa darasa la saba wawe na ufahamu zaidi juu ya chanzo kingine cha umeme ambacho ni rafiki wa mazingira kwa kupitia mafunzo katika madarasa yao katika hafla fupi iliyofanyika ofisini kwa Mh. Edward Lowassa jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkurugenzi wa Mauzo wa Hoteli ya DoulbeTree by Hilton Florenso Kirambata.

Mkurugenzi wa Kanda wa Hoteli ya DoubleTree by Hilton ya Dar es Salaam Bw. Judd Lehmann (katikati) akimkabidhi moja kati ya taa 200 zinazotumia nishati ya jua Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli Mh. Edward Lowassa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mauzo wa Hoteli ya DoulbeTree by Hilton Florenso Kirambata akishuhudia tukio hilo kwenye hafla fupi iliyofanyika Ofisini kwa Mh. Edward Lowassa jijini Dar.

Mkurugenzi wa Mauzo wa Hoteli ya DoulbeTree by Hilton Florenso Kirambata akikabidhi baadhi ya taa zinazotumia nishati ya jua kwa Kaimu Afisa Elimu wa Wilaya ya Monduli Jumanne Masuke. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Waziri Mkuu wa zamani Mh. Edward Lowassa ( wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Kanda wa Hoteli ya DoubleTree by Hilton ya Dar es Salaam Bw. Judd Lehmann (wa pili kushoto).

Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli Mh. Edward Lowassa akitoa shukrani kwa uongozi wa DoubleTree Foundation ambapo ametumia fursa hiyo kuitaka serikali kuwekeza sana katika elimu ili kuweza kukuza uchumi.Aidha amesema ni vyema kuwekeza katika sekta ya elimu ili tuweze kusonga mbele na kuwa na kizazi cha watu wenye elimu kwani masikini asiye na elimu ni hatari kuliko mtu yeyote, kwa kuwa mtu anapopata elimu anakuwa na ufahamu unaomuwezesha kukabiliana na maisha ya kila siku.



Picha juu na chini ni Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Monduli Mh. Edward Lowassa akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Kanda wa Hoteli ya DoubleTree by Hilton ya Dar es Salaam Bw. Judd Lehmann (katikati) na Kushoto ni Mkurugenzi wa Mauzo wa Hoteli ya DoulbeTree by Hilton Florenso Kirambata mara baada ya kukabidhiwa taa 200 zinazotumia nishati ya jua atakazozigawa katika jimbo lake kwa shule za msingi.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Arusha Forum - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger