Aliyepiga picha na Lema akamatwa, si mwanajeshi - Arusha Forum
Headlines News :
Home » » Aliyepiga picha na Lema akamatwa, si mwanajeshi

Aliyepiga picha na Lema akamatwa, si mwanajeshi

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Saturday, January 5, 2013 | 10:42 AM

Written by  Mwandishi wetu

Aliyejidai kuwa ni Mwanajeshi wa JWTZ kizuiziniJeshi la Wananachi JWTZ kwa kushirikiana na polisi limefanikiwa kumkamata kijana aliyejidai kuwa ni mwanajeshi wa jeshi hilo kikosi cha Monduli.

Kijana huyo alipiga picha na Mbunge wa Arusha Godbless lema alipokuwa akiwasalimia wananchi baada ya kurudishiwa ubunge wake na mahakama ya Rufani kitendo ambacho ni kosa kwa Mwanajeshi yeyote nchini kushabikia habari za vyama.

Aidha uchunguzi wa awali wa kipolisi umebaini kuwa Kijana huyo hakuwa mwanajeshi wa JWTZ kama alivyojitambulisha kwa viongozi wa Chadema na kwa waandishi wa habari bali aliwahi kuwa JKT na akaacha.

Uchunguzi huo pia umebaini kuwa Kijana huyo alikuwa akivaa nguo hizo za Kijeshi mara kwa mara kwa miaka mingi hivyo mkuwafanya wananchi wa Mererani kumtambua kuwa mwanajeshi.


Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Arusha Forum - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger