Mafuriko makubwa Mtwara, nyumba zajaa maji - Arusha Forum
Headlines News :
Home » » Mafuriko makubwa Mtwara, nyumba zajaa maji

Mafuriko makubwa Mtwara, nyumba zajaa maji

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Sunday, January 20, 2013 | 7:41 AM

 Written by  Mwandishi wetu
Maji yakiwa yamezingira nyumba mkoani Mtwara baada ya mvua kubwa kunyesha


Mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali imenyesha leo majira ya asubuhi  mkoani Mtwara na kusababisha mafuriko huku ikiwaacha watu wengi kukosa makazi.

Mvua hiyo inayodaiwa kunyesha kwa masaa manne imehatarisha maisha ya wananchi mkoani humo kufuatia kuharibu barabara, nyumba mazao na maeneo mengine ya biashara jambo linaloelezwa na wakazi wa eneo hilo kuwa imeongeza ugumu wa maisha.

Pamoja na kasi ya mvua hiyo iliyosababisha kujaa kwa maji katika maeneo mengi, taarifa za vifo bado hazijaelezwa ingawa wananchi wameomba msaada wa hali na mali kutoka kwa serikali ili kunusuru maisha yao katika kipindi hiki.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Arusha Forum - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger