Lema atiwa mbaroni kwa uchochezi baada ya kutoroka eneo la tukio - Arusha Forum
Headlines News :
Home » » Lema atiwa mbaroni kwa uchochezi baada ya kutoroka eneo la tukio

Lema atiwa mbaroni kwa uchochezi baada ya kutoroka eneo la tukio

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Friday, April 26, 2013 | 8:21 PM

“Kuna taratibu za kumwita mbunge polisi, wanaweza kunipigia simu au kuwasiliana na Spika, lakini siyo kutumia utaratibu huu wa kutangaza kwenye vyombo vya habari kuwa mimi natakiwa kukamatwa wakati najua sina kosa,”alisema Lema.

Polisi wanena

Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas jana, alikiri maofisa wa jeshi hilo kumkamata mbunge huyo juzi usiku na hadi jana mchana alikuwa bado yupo rumande.

“Ni kweli tupo naye hapa polisi, anasubiri kuhojiwa kutokana na tuhuma za uchochezi katika Chuo cha Uhasibu Arusha,”alisema Kamanda Sabas. Alisema uamuzi wa kuendelea kumshikilia au kumwachia, utatolewa baada ya kukamilika mahojiano.

Mapema wakili wa Lema, Hamphrey Mtui akizungumza na Mwananchi nje ya kituo kikuu cha polisi, alisema bado alikuwa hajaruhusiwa kuonana na mteja wake .

“Bado tunasubiri polisi wamtoe na wakati wa kuchukua maelezo yake ndiyo wameniambia wataniita,” alisema Mtui. Baadaye Lema alihojiwa lakini alikataliwa kupewa dhamana.

Taarifa za kukamatwa kwa Lema zilianza kusambaa juzi saa sita kasorobo usiku na ilipofika jana asubuhi tayari tukio hilo lilikuwa limeishateka mijadala ya mitandao ya kijamii.

Mijadala hiyo iliambatana na mkanda wa Video wa Lema wakati akizungumza na wananafunzi wa IAA.

Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Arusha Forum - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger