MHE. MEMBE AKUTANA NA UJUMBE WA WABUNGE KUTOKA UJERUMANI - Arusha Forum
Headlines News :
Home » » MHE. MEMBE AKUTANA NA UJUMBE WA WABUNGE KUTOKA UJERUMANI

MHE. MEMBE AKUTANA NA UJUMBE WA WABUNGE KUTOKA UJERUMANI

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Wednesday, February 13, 2013 | 11:52 AM

 Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Klaus-Peter Willsch, Kiongozi wa Ujumbe wa Wabunge wa Kamati ya Bajeti ya Bunge la Ujerumani alipokutana nae Wizarani kwa  mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Ujerumani.
 Mhe. Membe akimsikiliza Mhe. Willsch wakati wa mazungumzo yao.
 
 Mhe. Willsch (kulia kwa Waziri Membe) akimsikiliza Mhe. Membe wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Bajeti ya Bunge la Ujerumani pamoja na Mhe. Klaus-Peter Brandes ( wa sita kutoka kushoto), Balozi wa Ujerumani hapa nchini.
 
 Wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsilikiza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yake na Wabunge kutoka Ujerumani. Kutoka kushoto ni Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika,Bibi Zainab Angovi, Afisa kutoka Idara ya Ulaya na Amerika na Bw. Grayson Ishengoma, Afisa kutoka Idara ya Ulaya na Amerika.
 
 Mhe. Membe akifurahia Medali Maalum aliyokabidhiwa na Mhe. Willsch kama ishara ya kutambua ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Ujerumani.
 Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe huo.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Arusha Forum - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger